Kwa mujibu wa idara ya tarjama ya Shirika la Habari la Hawza, ripoti ya "Palestine Al-Yawm", Knesset ya Israeli ilipitisha mswada huo kwa kura 39 za ndiyo dhidi ya 16 za hapana katika mzunguko wa kwanza wa makubaliano.
Harakati ya Jihad Islami imesisitiza kuwa sheria hii inaonesha asili ya kibaguzi, ukandamizaji na ukatili wa utawala huo, na kuthibitisha kwamba taasisi zake zote, ikiwa ni pamoja na Knesset na mfumo wa mahakama, zimegeuka kuwa vyombo vya jinai vinavyotumia mateso dhidi ya taifa la Palestina.
Harakati hiyo iliongeza kuwa wakati vyombo vya usalama, jeshi la wapiganiaji wa kikoloni na wakazi wa vitongoji wanatekeleza mauaji dhidi ya watu wetu bila kuwa na mashauri au uwajibikaji wowote, kupitishwa kwa sheria hii ni jaribio la kuanzisha mfumo wa sheria mbili katika Ukingo wa Magharibi ambao unawaadhibu Wapalestina na kuwapa wakazi wa vitongoji na wavamizi kinga ya ukosefu wa adhabu.
Harakati ya Jihad Islami iliwasifu wale waliochukua msimamo wa kulaani kitendo hiki kipya cha jinai — ikimaanisha asasi na serikali zilizotoa kauli za kulaani — na kuitaka jumuiya ya kimataifa ichukue hatua madhubuti za kuzuia uhalifu huu unaoendelea.
Aidha, harakati hiyo ilitoa wito wa kuwashtaki na kuwaadhibu mawaziri na wabunge wa Knesset waliopiga kura ya ndiyo kwa mswada huo kwenye mahakama za kimataifa, ikisema kwamba kesi dhidi yao inapaswa kujumuisha tuhuma za kuchochea na kuendeleza uhalifu wa kivita.
Kwa kumalizia, harakati hiyo ilisisitiza kwamba wafungwa Wapalestina waliomo katika magereza ya utawala wa kikoloni ni amana mikononi mwa watu wa Palestina, na kwamba nguvu za upinzani hazitakoma kufanya jitihada zote za kuwaacha huru. Harakati hiyo pia iliwaomba Wapalestina kuongeza na kusisitiza aina zote za muqawama dhidi ya utawala huo.
Maoni yako